Shabaha

    Kufikia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:

    • Kueleza maana ya shina la neno
    • Kutaja sifa za shina la neno
    • Kutaja aina tatu za mashina
    • Kuelezea kuhusu aina tatu za mashina.

Kudurusu

    • Neno ni kitengo kidogo cha lugha. Huundwa kwa silabi ambazo zimefungamanishwa na kuleta maana.
    • Mzizi wa neno ni sehemu ya neno ambayo inabeba maana halisi ya neno. Sehemu hiyo ya neno haibadiliki hata neno linapowasilishwa katika kauli tofauti.
    • Aina mbili kuu za mizizi katika lugha ya Kiswahili ni:
      • Mzizi tegemezi
      • Mzizi huru.
    • Aina mbili za mzizi tegemezi ni:
      • Mzizi asilia
      • Mzizi mnyumbuliko.

Maagizo

    Kwa kutumia ubunifu na maneno yako mwenyewe, andika maelezo mafupi juu ya somo hili kwenye kitabu chako cha mazoezi unapoendelea kusoma na kisha uwasilishe maelezo yako kwa mwalimu wako wa lugha ya Kiswahili ili kuwezesha uhakiki na maoni yanayofaa.

Msamiati

    Beba: Carry

    Fungamanisha: Bind

    Gawa: Divide

    Halisi: Real

    Kauli: Statement

    Kiambishi: Affix

    Maana: Meaning

    Maoni: Comments/Feedback

    Msingi: Foundation

    Mzizi: Root of a word

    Neno: Word

    Rejelea: Refer

    Sehemu: Part

    Shina: Stem of a word

    Shina ambatani: Compound word

    Shina changamano: Root verb

    Shina sahili: Root word

    Sifa: Characteristics/Features

    Ubunifu: Creativity

    Uhakiki: Review

    Wasilisha: Present

    Wingi: Plural.

Module 3, Lesson 1
In Progress

Shina la neno

Module Progress
0% Complete

Shughuli 1: Maana ya shina

Shina ni neno lenye maana kamili, na ambalo haliwezi kugawanywa kwa misingi ya mzizi na viambishi. Neno lote ni mzizi.  Shina linaweza kusimana pekee na kuleta maana.

Wingi wa shina ni mashina.

Shughuli 2: Sifa za shina

Zifuatazo ni baadhi ya sifa za shina:

  • ni neno kamili
  • linaweza kusimama pekee yake na kuleta maana
  • linabeba maana halisi ya neno
  • linaweza kutumika lilivyo kama mzizi wa kuundia neno jipya
  • haliwezi kugawika zaidi bila kupoteza au kubadili maana ya neno.

Shughuli 3: Aina tatu za mashina

Aina tatu za mashina katika lugha ya Kiswahili ni:

  • Shina sahili
  • Shina changamano
  • Shina ambatani.

Shughuli 4: Shina sahili

Shina hili hurejelewa pia kama mzizi huru. Hili ni shina lililoundwa kwa mofimu huru moja tu yenye maana kamili. Ni neno huru ambalo haliwezi kugawika zaidi bila kupoteza maana yake.

Mifano:

shangazi

jana

rafiki

chupa

babu

kesho

nyanya

simba

kitabu

baba

nyumba

kalamu

Shughuli 5: Shina changamano

Hili ni shina lililoundwa kwa kufungamanisha mzizi wa neno na kiambishi tamati katika kauli ya kutenda ‘-a’.

Mifano:

pig+a

andik-a

lip-a

osh-a

chez-a

imb-a

fagi-a

tazam-a

lim-a

shik-a

beb-a

wek-a

Shughuli 6: Shina ambatani

Hili ni shina lililoundwa kwa kuambatanisha mofimu huru mbili, ambazo pamoja huwa mzizi wa neno.

Mifano:

mbwamwitu

babamkwe

mwanasayansi

wazimamoto

garimoshi

mwananchi

Zoezi

Quiz 1 of 0

Shina la neno