Shabaha

    Kufikia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:

    • Kueleza maana ya ala za sauti.
    • Kutaja aina mbili kuu za ala za sauti.
    • Kueleza tofauti kati ya aina mbili kuu za ala za sauti.
    • Kutoa mifano sahihi ya kila aina kuu ya ala za sauti.

Kudurusu

    Sauti ni mlio unaotokana na tamko. Ni kipashio kidogo zaidi cha lugha kisicho na maana.

Maagizo

    Kwa kutumia ubunifu na maneno yako mwenyewe, andika maelezo mafupi juu ya somo hili kwenye kitabu chako cha mazoezi unapoendelea kusoma na kisha uwasilishe maelezo yako kwa mwalimu wako wa lugha ya Kiswahili ili kuwezesha uhakiki na maoni yanayofaa.

Msamiati

    Ala: Instrument

    Ainisha: Classify

    Jumuisha: Include/Comprise

    Kidogo: Small

    Kipashio: Piece/Element

    Kundi: Group

    Lugha: Language

    Shughuli: Activity

    Sogea: Move

    Tamka: Pronounce

    Viungo: Parts.

Module 1, Lesson 1
In Progress

Ala za sauti

Module Progress
0% Complete

Shughuli 1:  Maana ya ala za sauti

Kutamka ni kule kutoa kwa sauti za maneno ya lugha fulani kinywani.

Ala za sauti ni viungo vya mwili ambavyo vinatumiwa kutamkia sauti. 

Picha ifuatayo inaonyesha ala mbali mbali za sauti.

Kumbuka: Midomo ni miwili (mdomo wa juu, na mdomo wa chini).

Shughuli 2:  Aina kuu za ala za sauti

Ala za sauti zinaweza kuanishwa katika makundi mawili yafuatayo:

  • ala sogezi
  • ala tuli.

Shughuli 3: Ala sogezi

Kundi hili linajumuisha viungo vya kutamkia ambavyo husogeasogea wakati sauti inapotamkwa. 

Midomo

Ulimi

Shughuli 4: Ala tuli

Kundi hili linajumuisha viungo vya kutamkia ambavyo havisogeisogei wakati sauti inapotamkwa. 

Mifano ya ala tuli

Kaakaa gumu

Kaakaa laini

Fizi

Meno

Shughuli 5: Wimbo kuhusu ala za sauti.

Kariri wimbo ufuatao ili kukusaidia kukumbuka kwa urahisi ala tofauti za sauti.

ALA ZA SAUTI


Umio wa hewa
Nyuzi za sauti
Chemba cha kinywa
Chemba cha pua
Kidakatonge
Kaakaa laini
Ulimi, Pua
Kaakaa gumu
Ufizi, Meno
na Midomo
ni Ala Za Sauti.

Zoezi

Quiz 1 of 0

Ala za sauti