Shabaha

    Kufikia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:

    • Kutambua herufi za alfabeti ya Kiswahili.
    • Kukariri sauti za alfabeti ya Kiswahili.
    • Kuimba wimbo wa alfabeti ya Kiswahili
    • Kutaja aina mbili kuu za sauti za Kiswahili.
    • Kujibu maswali kuhusu alfabeti ya Kiswahili kwa usahihi.

Maagizo

    Kwa kutumia ubunifu na maneno yako mwenyewe, andika maelezo mafupi juu ya somo hili kwenye kitabu chako cha mazoezi unapoendelea kusoma na kisha uwasilishe maelezo yako kwa mwalimu wako wa lugha ya Kiswahili ili kuwezesha uhakiki na maoni yanayofaa.

Msamiati

    Shughuli: Activity

    Alfabeti: Alphabet

    Andika: Write

    Sauti: Sound

    Sehemu: A part of

    Herufi: Letter of the alphabet

    Gawika: Broken

    Kwa utaratibu maalum: In a special order

    Jumla ya: A total of

    Jumuisha: Consists of

    Changamano: Complex

    Shughuli: Activity

    Husisha: Associate/relate

    Dhihirishwa – Manifested / shown

    Kariri: Memorize

    Ubunifu: Creativity

    Alama: Mark.

Module 1, Lesson 3
In Progress

Alfabeti ya Kiswahili

Module Progress
0% Complete

Shughuli 1:  Alfabeti ya Kiswahili

Sauti ni sehemu ndogo kabisa ya neno ambayo haiwezi kugawika zaidi, na hudhihirishwa kwa mlio unaotokana na tamko.

  • Sauti huandikwa kwa kutumia alama zinazoitwa herufi.
  • Jumla ya herufi za lugha ambazo zimepangwa kwa utaratibu maalum uliokubaliwa huitwa Alfabeti.
  • Alfabeti ya Kiswahili inajumuisha herufi thelathini.
  • Kila herufi ya alfabeti ya Kiswahili inahusishwa na sauti moja tu.

Shughuli 2:  Kukariri kwa alfabeti ya Kiswahili

Jifunze wimbo wa alfabeti ufuatao kisha uutumie kuandaa ngoma maalum ya kuburudisha wanafunzi wengine darasani.

Shughuli 3: Alfabeti kamili ya Kiswahili

Andika alfabeti ya Kiswahili katika kitabu chako cha mazoezi.

a

b

ch

d

dh

e

f

g

gh

h

i

j

k

l

m

n

ng’

ny

o

p

r

s

sh

t

th

u

v

w

y

z

Kumbuka: Alfabeti ya Kiswahili haina herufi c, q, na x.

Zoezi

Quiz 1 of 0

Alfabeti ya Kiswahili