Shabaha

    Kufikia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:

    • Kutaja irabu zote za Kiswahili.
    • Kuimba wimbo wa irabu za Kiswahili.
    • Kutaja na kuandika alfabeti ya Kiswahili kwa mpangilio sahili.
    • Kujibu maswali kuhusu sauti za Kiswahili kwa usahihi.

Kudurusu

    • Sauti ni kipashio kidogo kabisa cha neno ambacho kinaweza kutamkwa, lakini hakiwezi kugawika zaidi.
    • Herufi ni alama ambazo zinatumiwa kuandika sauti.
    • Alfabeti ni jumla ya herufi za lugha ambazo zimepangwa kwa utaratibu maalum.
    • Alfabeti ya Kiswahili ina herufi thelathini.
    • Kila herufi ya alfabeti ya Kiswahili inahusishwa na sauti moja tu.
    • Alfabeti ya Kiswahili haina herufi c, q, na x.
    • Aina mbili kuu za sauti katika alfabeti ya Kiswahili ni irabu na konsonanti.
    • Alfabeti kamili ya Kiswahili ni:

    A, b, ch, d, dh, e, f, g, gh, h, i, j, k, l, m, n, ng’, ny, o, p, r, s, sh, t, th, u, v, w, y, z.

Maagizo

    Kwa kutumia ubunifu na maneno yako mwenyewe, andika maelezo mafupi juu ya somo hili kwenye kitabu chako cha mazoezi unapoendelea kusoma na kisha uwasilishe maelezo yako kwa mwalimu wako wa lugha ya Kiswahili ili kuwezesha uhakiki na maoni yanayofaa.

Msamiati

    Alama: Mark.
    Alfabeti: Alphabet
    Gawika: Broken
    Herufi: Letter of the alphabet
    Husisha: Associate/relate
    Irabu/vokali/Voweli: Vowel
    Jumla ya: A total of
    Kariri: Memorize
    Kipashio: A piece/part
    Konsonanti: Consonant
    Kwa utaratibu maalum: In a special order
    Makundi: Groups
    Rejelea: Refer
    Sauti: Sound
    Shughuli: Activity
    Ubunifu: Creativity

Module 1, Lesson 2
In Progress

Voweli za Kiswahili

Module Progress
0% Complete

Shughuli 1:  Voweli za Kiswahili

Irabu ni aina ya sauti katika alfabeti ya Kiswahili.

  • Irabu za Kiswahili hurejelewa kwa majina mengine kama vokali na voweli.
  • Kuna jumla ya irabu tano (5) katika alfabeti ya Kiswahili.
  • Irabu za Kiswahili huandikwa kwa herufi zifuatazo:

Shughuli 2:  Kukariri Voweli za Kiswahili

Imba wimbo ufuatao kwa pamoja ili kukariri voweli za Kiswahili.

Shughuli 3: Andika alfabeti ya Kiswahili

Quiz 1 of 0

Voweli za Kiswahili

Zoezi

Quiz 1 of 0

Voweli za Kiswahili