Shabaha

    Kufikia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:

    • Kueleza maana ya silabi.
    • Kutaja sifa bainifu za silabi katika lugha ya Kiswahili.
    • Kueleza tofauti kati ya silabi na sauti.
    • Kueleza jinsi ya kutambua silabi katika neno.
    • Kueleza umuhimu wa silabi.

Kudurusu

    • Sauti ni sehemu ndogo kabisa ya neno ambayo haiwezi kugawika zaidi, na hudhihirishwa kwa mlio unaotokana na tamko.
    • Sauti mbili kuu za lugha ya Kiswahili ni irabu na konsonanti.
    • Herufi ni alama zinazotumiwa kuandika sauti za lugha ya Kiswahili.
    • Sauti huandikwa kwa kutumia herufi ndogo pekee.
    • Alama za mshazari zinapowekwa pande zote mbili za herufi katika andiko huonyesha kuwa andiko hilo ni la sauti.

Maagizo

    Kwa kutumia ubunifu na maneno yako mwenyewe, andika maelezo mafupi juu ya somo hili kwenye kitabu chako cha mazoezi unapoendelea kusoma na kisha uwasilishe maelezo yako kwa mwalimu wako wa lugha ya Kiswahili ili kuwezesha uhakiki na maoni yanayofaa.

Msamiati

    Alama ya kijistari: Hyphen

    Andika: Write

    Dhihirisha: Manifest/Show

    Fungu: Part

    Jumuisha: Comprise/Include

    Kati ya: Between

    Kopa: Borrow

    Lugha: Language

    Maana: Meaning

    Mchanganyiko: A combination

    Moja: One

    Muhimu: Important

    Neno: Word

    Onyesha: Show

    Pigo la sauti: A sound beat

    Rejelea: Refer

    Sauti: Sound

    Sehemu: A part of

    Sifa bainifu: Characteristic features

    Silabi: Syllable

    Tahajia: Spelling

    Tambua: Recognize/Realize

    Tamka: Pronounce

    Tenganisha: Separate

    Tumia: Use

    Unganisha: Connect.

Module 2, Lesson 1
In Progress

Maana ya silabi

Module Progress
0% Complete

Shughuli 1:  Maana ya silabi   

  • Silabi ni sehemu ya neno ambayo inatamkika kama tamko moja la sauti. Hurejelewa kwa namna nyingine kama pigo la sauti katika neno.
  • Silabi za Kiswahili zinaweza kuhesabika.
  • Njia moja ya kutambua silabi katika neno fulani ni kwa kuhusisha kila sauti ya kipekee inayotamkwa na pigo moja, ifuatavyo:

Neno

Silabi katika neno

Kuhesabu silabi

Jumla ya mapigo

Kiswahili

ki-swa-hi-li

4

silabi

si-la-bi

3

sauti

sa-u-ti

3

kinatamkwa

ki-na-ta-m-kwa

5

mchanganyiko

m-cha-nga-nyi-ko

5

konsonanti

ko-nso-na-nti

4

Kumbuka: Alama ya kijistari, hutumiwa kutenganisha silabi za neno.

Shughuli 2:  Sifa bainifu za silabi katika lugha ya Kiswahili

Katika lugha ya Kiswahili silabi:

  • ni sehemu au kitengo kimoja cha neno.
  • inatamkwa kama tamko moja lisilokatika la sauti
  • inaweza kujumuisha mchanganyiko wa vokali na konsonanti.
  • inaweza kujumuisha herufi moja au zaidi ya alfabeti ya Kiswahili.
  • Ina sauti moja tu

Jedwali lifuatalo linajumuisha vielelezo vya sifa za silabi:

Herufi

Silabi

Tamko

e

=

e

m

=

m

m + e

=

me

m + b + e

=

mbe

m + b + w + e

=

mbwe

Shughuli 3: Umuhimu wa silabi katika lugha ya Kiswahili

  • Silabi hutumiwa katika uundaji wa maneno ya Kiswahili.
  • Silabi hurahisisha:
    • kutamkwa kwa maneno.
    • kusomwa kwa maneno.
    • kuandikwa kwa maneno.
    • kutahajia maneno.

Zoezi

Quiz 1 of 0

Maana ya silabi