Shabaha

    Kufikia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze:

    • Kueleza dhima ya International Phonetic Alphabet (IPA)
    • Kutambua shirika linalodhibiti IPA
    • Kueleza mahali pa kupata IPA mtandaoni
    • Kueleza jinsi ya kutumia IPA kubaini sauti za maneno.

Kudurusu

    • Sauti ni sehemu ndogo kabisa ya neno ambayo haiwezi kugawika zaidi, na hudhihirishwa kwa mlio unaotokana na tamko.
    • Silabi ni pigo la sauti.
    • Neno ni kitengo kidogo cha lugha. Huundwa kwa silabi ambazo zimefungamanishwa na kuleta maana.

Maagizo

    Kwa kutumia ubunifu na maneno yako mwenyewe, andika maelezo mafupi juu ya somo hili kwenye kitabu chako cha mazoezi unapoendelea kusoma na kisha uwasilishe maelezo yako kwa mwalimu wako wa lugha ya Kiswahili ili kuwezesha uhakiki na maoni yanayofaa.

Msamiati

    Agizo: Instruction

    Alfabeti ya Kifonetiki: Phonetic Alphabet

    Ainisha: Classify

    Baini: Find out/Establish

    Bofya: Click

    Chapisha: Publish

    Dhibiti: Control

    Dhima: Function

    Geni: Alien/New

    Julikana: Known

    Jumuishi: Integrated

    Kiungo: Link

    Konsonanti: Consonant

    Maalum: Special

    Maana: Meaning

    Makini: Carefully/attentively

    Maoni: Comments/Feedback

    Matamshi: Pronunciation

    Mfumo: System

    Miongoni: Among

    Mtandao: Internet

    Neno: Word

    Orodha: List

    Rahisi: Easy

    Rejelea: Refer

    Sahihi: Correct

    Sanifisha: Standardize

    Sarufi: Grammar

    Sauti: Sound

    Sawa: Same/Equivalent

    Sehemu: A part of

    Shirika: Organization

    Shughuli: Activity

    Silabi: Syllable

    Tafsiri: Translate

    Tahajia: Spelling

    Tambua: Recognize/Realize

    Tamka: Pronounce

    Tegemea: Depend on

    Tembelea: Visit

    Tofauti: Different

    Ubunifu: Creativity

    Uhakiki: Review

    Ulimwengu: The Word

    Voweli: Vowel

    Wakilisha: Represent

    Wezesha: Enable

    Zaidi: More

    Zingatia: Consider/Focus on.

Module 4, Lesson 1
In Progress

International Phonetic Alphabet

Module Progress
0% Complete

Shughuli 1: Dhima ya International Phonetic Alphabet (IPA)

International Phonetic Alphabet (IPA) ni mfumo maalum unaowezesha watu kote ulimwenguni kutambua sauti mbali mbali zinazotumika katika matamshi kwa urahisi, na kuzitamka kwa usahihi na kwa njia sawa.   

Katika alfabeti hii, sauti za kifonetiki zinawakilishwa na ishara maalum ambazo zimesanifishwa.

Kila sauti tofauti ina ishara yake maalum. Ishara sahihi hutambuliwa kwa kusikiliza sauti inapotamkwa kwa makini. Haitegemei tahajia ya neno.  

Sauti zinazopatikana katika lugha ya Kiswahili ni miongoni mwa sauti ambazo zimeorodheshwa katika International Phonetic Alphabet.

Shughuli 2: Uzalishaji na udhibiti wa International Phonetic Alphabet

Mambo yanayozingatiwa katika fonetiki yanajumuisha kuzalisha, kutamka, kusambaza, kupokea na kuainisha sauti. Shirika ambalo lina jukumu la kuandaa, kuchapisha, na kusimamia alfabeti ya kifonetiki ya kimataifa ni International Phonetic Association. 

Kwa habari zaidi kuhusu International Phonetic Association na kazi zake, bofya kiungo kifuatacho:

Shughuli 3: Orodha kamili ya sauti katika International Phonetic Alphabet (IPA)

Alfabeti ya kifonetiki imechapishwa katika sehemu mbili, ambazo ni konsonanti na voweli.

  • Bofya kiungo kifuatacho ili kuona sauti zote za konsonanti ambazo zimeorodheshwa katika International Phonetic Alphabet.
  • Bofya kiungo kifuatacho ili kuona sauti zote za voweli ambazo zimeorodheshwa katika International Phonetic Alphabet.

Shughuli 4: Jinsi ya kutumia International Phonetic Alphabet kubaini sauti za maneno

Unapokutana na neno geni ambalo maana na matamshi yake hayajulikani, unaweza:  

  1. kwanza kurejelea kamusi jumuishi ya lugha husika ili kubaini maana ya neno hilo na ishara zake za kifonetiki, halafu
  2. ukirejelea International Phonetic Alphabet (IPA), utafsiri ishara za neno ili kupata sauti na hivyo matamshi yake sahihi.

Zoezi

Quiz 1 of 0

International Phonetic Alphabet