Description
Shughuli 1: Makundi ya maneno ya Kiswahili
Maneno ya Kiswahili yanaweza kuanishwa katika makundi nane yafuatayo:
nomino
kielezi
Kiwakilishi
Kihusishi
Kivumishi
Kiunganishi
Kitenzi
Kihisishi
Shughuli 2: Aina nane za maneno katika lugha ya Kiswahili na lugha ya Kiingereza
Jedwali lifuatalo linaangazia aina za maneno katika lugha ya Kiswahili, sawa na jinsi makundi hayo yanavyorejelewa katika lugha ya Kiingereza.
Kiswahili (Umoja)
Kiswahili (Wingi)
Kiingereza/English
Nomino
Nomino
Noun
Kiwakilishi
Viwakilishi
Pronoun
Kivumishi
Vivumishi
Adjective
Kitenzi
Vitenzi
Verb
Kielezi
Vielezi
Adverb
Kihusishi
Vihusishi
Preposition
Kiunganishi
Viunganishi
Conjunction
Kihisishi
Vihisishi
Interjection
Shughuli 3: Zoezi
Kariri wimbo ufuatao ili kukusaidia kukumbuka kwa urahisi makundi nane ya aina za maneno.
Aina nane za maneno ya Kiswahili
Noun ni Nomino
Pronoun Kiwakilishi
Adjective Kivumishi
Verb Kitenzi
Adverb Kielezi
Preposition Kihusishi
Conjunction Kiunganishi
Interjection Kihisishi.
Reviews
There are no reviews yet.