Ala za sauti

KShs 20.00

-
+

Specs

Category:

Description

Shughuli 1:  Maana ya ala za sauti

Kutamka ni kule kutoa kwa sauti za maneno ya lugha fulani kinywani.

Ala za sauti ni viungo vya mwili ambavyo vinatumiwa kutamkia sauti. 

Picha ifuatayo inaonyesha ala mbali mbali za sauti.

Kumbuka: Midomo ni miwili (mdomo wa juu, na mdomo wa chini).

Shughuli 2:  Aina kuu za ala za sauti

Ala za sauti zinaweza kuanishwa katika makundi mawili yafuatayo:

  • ala sogezi
  • ala tuli.

Shughuli 3: Ala sogezi

Kundi hili linajumuisha viungo vya kutamkia ambavyo husogeasogea wakati sauti inapotamkwa. 

Midomo

Ulimi

Shughuli 4: Ala tuli

Kundi hili linajumuisha viungo vya kutamkia ambavyo havisogeisogei wakati sauti inapotamkwa. 

Mifano ya ala tuli

Kaakaa gumu

Kaakaa laini

Fizi

Meno

Shughuli 5: Wimbo kuhusu ala za sauti.

Kariri wimbo ufuatao ili kukusaidia kukumbuka kwa urahisi ala tofauti za sauti.

ALA ZA SAUTI


Umio wa hewa
Nyuzi za sauti
Chemba cha kinywa
Chemba cha pua
Kidakatonge
Kaakaa laini
Ulimi, Pua
Kaakaa gumu
Ufizi, Meno
na Midomo
ni Ala Za Sauti.

Zoezi

Back to Course

Ala za sauti

0% Complete
0/0 Steps
Quiz 1 of 0

Ala za sauti

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Ala za sauti”