Maana na dhima za vitenzi

KShs 20.00

-
+

Specs

Category:

Description

Shughuli 1: Maana ya vitenzi

  • Vitenzi ni maneno yanayorejelea vitendo.
  • Vitenzi ni mojawapo ya aina nane za maneno katika lugha ya Kiswahili.   

Shughuli 2: Dhima za vitenzi

Vitenzi vina uamilifu tofauti wa kisarufi. Zifuatazo ni baadhi ya dhima za vitenzi.

a)   Vitenzi huashiria vitendo, matukio, au hali za kuwa kwa vitu

Watoto wanakimbia.
The children are running.

Kunanyesha
It is raining.

Hawa ni watoto.
These are children.

b)   Vitenzi huwezesha uundaji wa vishazi vinavyoleta maana

  • Kishazi ni fungu la maneno lenye kiima kimoja na kiarifa kimoja. Wingi wa kishazi ni vishazi.
  • Kishazi huru huhitaji tu kiima kimoja na kiarifu kimoja ili kuleta maana.
  • Sentensi inaweza kuundwa kwa kutumia kishazi kimoja, au vishazi zaidi ya moja.

  • Mtoto analala. (The baby is sleeping).
  • Maria atanunua kitabu kesho. (Maria will buy a book tomorrow).
  • Mwashi alijenga nyumba tatu. (The mason built three houses).
  • Watoto walifurahii walipokuwa wakicheza. (The children were happy when they were playing).

c)   Vitenzi huwezesha uwasilishaji wa nyakati na vipengele vinavyohusiana na wakati.

Vitenzi vinaweza kurekebishwa kwa kutumia mbinu kama vile unyambulishaji, uambatanishaji, au kwa kuviongezea vitenzi visaidizi, ili kuwasilisha

  • nyakati tofauti
  • vipengele vinavyohusiana na wakati kama vile hali ya kukamilika kwa kitendo, muda wa kitendo, au kurudia kwa kitendo.

Nyakati / Hali

Mifano katika sentensi

Nyakati tofauti

Mama anapika ugali. (Mother is cooking ugali.)

Mama alipika ugali. (Mother cooked ugali.)

Mama atapika ugali. (Mother will cook ugali.)

Hali ya mazoea

Mama hupika ugali jioni. (Mother cooks ugali in the evening.)

Hali timilifu

Mama amepika ugali. (Mother has cooked ugali.)

d)   Vitenzi huwezesha uwasilishaji wa dhamira na mtazamo wa msemaji/mwaandishi

Vitenzi vinaweza kutumiwa kuwasilisha dhana mbalimbali kama vile; pendekezo, uwezo, wajibu, ushauri, mwaliko, ombi, hitimisho, agizo, uwezekano, ulazima, ruhusa, na kutoidhini.

Alama za uakifishaji hutumiwa katika maandishi kuwashilisha baadhi ya dhana hizi.

Dhana

Mifano katika sentensi

Ombi

Ninaweza kuimba nyimbo mbili? (May I sing two songs?)

Agizo

Imba! (Sing!)

Uwezo

Ninaweza kuandika vizuri. (I can write well.)

Wajibu

Unapaswa kuhudhuria mkutano. (You should attend the meeting.)

Ruhusa

Unaweza kwenda nyumbani.  (You can go home).

e) Vitenzi huwezesha makubaliano ya kisarufi.

Katika lugha ya Kiswahili, ngeli za nomino zilizo katika sentensi fulani huathiri miundo ya aina zingine za maneno ambayo yanahusiana nazo, kama vile; vitenzi, vivumishi, na vimilikishi.

Kwa kuchukua viambishi tofauti kama vile ambavyo vinaonyesha ngeli za nomino pamoja na idadi, vitenzi huwezesha uundaji wa sentensi zilizo sahihi kisarufi.

  • Mwanafunzi alisoma kitabu. (The student read a book.)
  • Wanyama wanalala. (The animals are sleeping.)
  • Kiti kilivunjika. (The chair broke.)
  • Mti una matunda. (The tree has fruits.)
  • Nguo zimekauka. (The clothes are dry.)

Reviews

There are no reviews yet.

Be the first to review “Maana na dhima za vitenzi”